0
DANSA wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Mose Iyobo ambaye anatajwa kuwa mpenzi wa msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ameshikwa na kigugumizi kuhusu tuhuma za kumpachika mimba Aunt ambaye ni mke wa mtu.
Dansa wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Mose Iyobo akiwa na Aunt Ezekiel.

Mose alionesha kigugumizi hicho baada ya kutaitiwa na paparazi wetu akiulizwa anajisikiaje kumpachika mimba mke wa mtu na vipi kama mume wa Aunt anayedaiwa kufungwa huko Dubai ataachiwa huru na kurudi.“Aaahhaa.. Mhh..Hayoo ni ya Aunt mwenyewe mimi hayanihusu,” alisema Mose kisha kimya kirefu kikafuatia kabla ya kuikata simu yake.
-GPL

Post a Comment

 
Top