JAMAA
anayedaiwa kwamba ni mpambe mkubwa wa mmoja wa wagombea urais mwakani
ambaye ni fundi wa kufunga madishi, mkazi wa Magomeni-Makanya jijini Dar
es Salaam, almaarufu Mgosingwa, amejikuta akivishwa shanga baada ya
kunaswa na mke wa mtu chumbani kwake.
Mgosingwa akivishwa shanga baada ya kufumaniwa na mke wa mtu. FUMANIZI
Tukio hilo la aina yake la kufungia mwaka 2014 lilijiri kwenye
fumanizi la jamaa huyo lililochukua nafasi nyumbani kwake maeneo ya
Magomeni-Makanya, Dar, Jumanne iliyopita ambapo alifumwa na mke wa jamaa
aliyejitambulisha kwa jina moja la Faki aitwaye Mwanahamisi akidaiwa
kumrubuni kwa nguo za Sikukuu ya Krismasi.
Kwa mujibu wa mwenye mke, baada ya Mgosingwa ambaye mkewe alikuwa
safarini, kunaswa laivu alitaka kuchoropoka kupitia dirishani lakini
jamaa alimkamata miguu na kumrudisha ndani.
OFM
Kama kawa, makamanda wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global
Publisher wanaotumia bodaboda ziendazo kasi, walitonywa na kufanikiwa
kufika eneo la tukio ndani ya dakika sifuri.
...Akiwasihi
wamuachie baada ya kufumaniwa. OFM walipofika walikuta mtiti umeshika
kasi ambapo kabla ya kufikia hatua ya kudhuriana, polisi waliokuwa doria
mtaani waliitwa na wasamaria wema na kwenda kuokoa jahazi.
AVISHWA SHANGA
Polisi walipofika walimkuta mwenye mke akiwa na shanga mkononi
akimvalisha Mgosingwa ambaye tayari hakuwa na ujanja.Hata hivyo, polisi
hao walifanya kazi ya ziada kumdhibiti mwenye mke ambaye alikuwa
akipambana nao akitaka aachiwe apambane na mgoni baada ya kumvisha
shanga.
MAYOWE
“Niacheni jamani lazima na mimi leo nim….(tusi), haiwekani kabisa mtu atake kumdhalilisha mke wangu.
“Mke wangu nitajua cha kumfanya tukifika nyumbani, yaani ukweli nampenda sana mke wangu,” alisikika mwenye mke akipiga mayowe.
WAAMRISHWA WAVAE NGUO
Tukio hilo lilisababisha mjumbe wa nyumba kumi wa eneo hilo
aliyejitambulisha kwa jina la Mama Vicky na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa
Makanya (hakutaja jina) wafike eneo hilo na kuwaamrisha waliofumaniwa
wavae nguo kwanza.
SERIKALI YA MTAA
Baada ya kuvaa, wahusika wote walipelekwa kwenye ofisi ya mtendaji wa
mtaa huo ili wazungumze na ikiwezekana wayamalize kwani wahusika hao
walikuwa ‘hawajaduu’ bado.
MSAMAHA
Baada ya kufika ofisi ya mtendaji, Mgosingwa alimpigia magoti mwenye
mke na kumuomba msamaha huku akikiri kuwa alikuwa akitaka kula tunda la
mkewe lakini alikuwa bado hajathubutu kufanya hivyo hata siku moja.
“Chondechonde kaka, mimi ni mwanaume mwenzako na wote, mimi, wewe na
mkeo tunatoka pamoja pale Makorora (Tanga) na familia zetu zinajuana
fika.“Naomba unisamehe ndugu yangu niko tayari kukulipa fidia ya
kunishika ugoni,” aliomba Mgosingwa.
Mgosingwa aliendelea kuomba radhi ambapo mjumbe wa nyumba kumi na
afisa mtendaji walimshauri mwenye mke kupunguza jazba kisha akubali
kuzungumza na mgoni wake, wasifike mbali na kuyamaliza ili kuepusha
usumbufu.
FAINI MIL. 1.5
Baada ya kushauriwa kwa muda mrefu, mwenye mke aliiheshimu mamlaka
hiyo ya serikali na kukubali kulipwa faini shilingi milioni moja na nusu
za Kitanzania ili kumsamehe mgoni na kumpa onyo kali endapo
wataendeleza kamchezo hako.Baada ya hapo, Mgosingwa aliendelea kuwapigia
simu ndugu zake wamtumie fedha kwenye simu ili amalize tatizo hilo.
NI MPAMBE WA MGOMBEA GANI?
Kwa mujibu wa majirani wa Mgosingwa ni mpambe wa mmoja wa wanasiasa
maarufu anayedaiwa kuwa kwenye ‘resi’ za kugombea urais mwakani,
kufumaniwa kwake kumetajwa pia kama ni njia mojawapo ya kumchafua
mgombea huyo.Mgosingwa alipoulizwa kama ni mpambe wa mgombea gani hakuwa
tayari kutaja.
Baadhi ya vigogo wanaotajwa kutaka kugombea urais kwenye Uchaguzi
Mkuu 2015 ambao wana wapambe kila kona Bongo ni pamoja na Mizengo Pinda,
Benard Membe, January Makamba, Frederick Sumaye, Dk. Khamis Kigwangala,
Dk. Wilbrod Slaa, Wiliam Ngeleja, Steven Wasira, Dk. Mohamed Shein, Dk.
Emmanuel Nchimbi, Dk. Asha-Rose Migiro na Edward Lowassa.
GPL
Post a Comment