Pichani
ni mwimbaji nyota wa muziki wa dansi Christian Bella akiwa na kaka yake
katikati ya jiji la Amsterdam nchini Holland tayari kwa onyesho lake
jijini humo.
Katika
onyesho hilo litakalofanyika Jumamosi hii, Christian Bella
atashirikiana na kaka yake Zoe Bella (pichani kushoto) ambaye ni
mwimbaji wa kiwango cha kimataifa.
Zoe Bella aliwahi kuimba kwenye bendi ya Koffi Olomide, Quartier Latin.
Bella
ameiambia Saluti5 kuwa anajaribu kuutangaza muziki wa dansi kutoka
Tanzania katika nchi kadhaa za Ulaya ili kufungua milango kwa wasanii
wengine wa dansi, hasa kutokana na ukweli kuwa soko la muziki huo ni
dogo sana.
Post a Comment