0

Msanii wa muziki kutoka Kenya, Jaguar ameweka wazi hisia zake za kumkubali sana staa wa filamu Irene Uwoya kutoka Bongo, ambapo amesema anajipanga kutua Bongo mwishoni mwa mwaka huu kuja kumuona staa huyu anayevutiwa naye.

Jaguar
Jaguar ameiambia E-Newz ya Eatv kuwa akitua Bongo hataishia kumuona Irene tu, bali atakwenda hadi kwa wazazi wa staa huyu kwa lengo ambalo hajalifafanua zaidi.
“Mimi naona nitue Tanzania, sijui nije December, sijui nimuijie Irene Uwoya, nije kumchukua, mwambie naja kumchukua, ameniambia nione wazazi kwanza, naja December kumchukua,” alisema Jaguar.
Irene Uwoya
Baada ya kauli hiyo Bongo5 ilimtafuta Uwoya na kuzungumzia ujio huo wa Jaguar ambao amesema anaufahamu, na akadai anakuja kufanya mipango ya kumuoa.
“Tunampango wa kuoana, bado anakuja,” alisema Irene Uwoya huku alifurahi. KUONA VIDEO BOFYA HAPA

Post a Comment

 
Top