 Kama
 ulibahatika kuona picha katika mitandao ya kijamii ikimwonyesha Miss 
Tanzania 2006 ambaye pia ni mwigizaji, Wema Sepetu akiwa na nyota wa 
filamu kutoka Ghana, Van Vicker wawili hao wapo katika matayarisho ya 
filamu mpya imedhibitishwa.
Kama
 ulibahatika kuona picha katika mitandao ya kijamii ikimwonyesha Miss 
Tanzania 2006 ambaye pia ni mwigizaji, Wema Sepetu akiwa na nyota wa 
filamu kutoka Ghana, Van Vicker wawili hao wapo katika matayarisho ya 
filamu mpya imedhibitishwa.
Mkali huyo wa filamu Afrika Magharibi alithibitisha hilo, kupitia 
mtandao wa kijamii wa Twitter huku akimsifia mlimbwende huyo kwamba ni 
mwigizaji mzuri.
“Kitu changu kingine kikubwa, nimefurahia muunganiko baina ya Ghana 
na Tanzania, ni siku ya kwanza lakini nimefurahishwa na namna 
tulivyoweza kuifanya kazi hii kwani unajua nini unakitaka. Nimefarijika 
kufanya kazi na wewe, katika filamu hii itakayojulikana kwa jina la ‘Day
 After Death’, mhusika mkuu ni Wema Sepetu na mimi,” aliandika katika 
mtandao wa huo alfajiri ya jana.Kusoma zaidi bofya
Van Vicker aliweka wazi kuwa filamu hiyo aliyoiongoza, ilimpa wakati 
mgumu lakini anafurahia changamoto alizopewa na mlimbwende huyo.
“Katika filamu hii watazamaji pia watawaona mabinti zangu wawili ambao wameigiza ndani yake.”
Meneja wa Wema, Martin alisema kuna kazi kadhaa zinazofanywa chini ya Kampuni ya Endless Fame na kampuni ya Van Vicker kwa sasa.
“Van Vicker kupitia kampuni yake ya Sky + Orange Productions ambayo 
yeye ni mkurugenzi mkuu na Wema kupitia Endless Fame akiwa mkurugenzi 
mkuu pia, wameungana kufanya mradi na tayari wameshafika nchini Ghana 
kwa ajili ya kukamilisha kazi hizo,” alisema Kadinda na kuongeza: “Huu 
ni mradi mkubwa ambao wanauandaa utakaojumuisha kampuni hizi mbili, kwa 
hiyo mashabiki wake wategemee makubwa inaweza kuwa filamu au vinginevyo 
wasubiri matokeo, Wema ameongozana na Petitman mmoja kati ya wafanyakazi
 wa kampuni.”
Wema aliandika katika ukurasa wake wa Instagram: “Tupo katika matayarisho.”
Chanzo:Mwananchi
 
Post a Comment