Aliyekuwa
 Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu katika pozi na mshindi wa pili, 
Lillian Kamazima (kulia) pamoja na mshindi wa tatu, Jihhan Dimachk.
Mshindi
 wa Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu, kwa hiari yake mwenyewe bila 
kulazimishwa na mtu ameamua kulivua rasmi taji hilo la urembo.

Akiongea na
 EATV mratibu wa shindano hilo Hashimu Lundenga amesema kuwa Sitti 
Mtemvu ameamua kwa maamuzi yake binafsi na sio wao kama kamati ya Miss 
Tanzania.
"Sababu
 kubwa ya Sitti kulivua taji hilo ni baada ya kuchoshwwa na maneno mengi
 yaliyozushwa juu yake, maana pia aliitwa na RITA kwaajili ya uchunguzi 
zaidi hivyo ameona mambo yanazidi kuzushwa mengi hivyo ameamua kulivua 
taji hilo". Amesema Hashimu Lundenga
Baada ya Sitti Mtemvu kulivua taji hilo atavalishwa aliyekuwa mshindi wa pili Lilian Kamazima
 
Post a Comment